Jamii
Jamii
Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
((وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَآ أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيمًا)) ((وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا))
((Na Mola wako Ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa heshima)) ((Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu, Warehemu kama walivyonilea utotoni)) [Al-Israa:23-24]
<?xml encoding="utf-8" ?>
‘Amali Za Kuwatendea Wazazi Waliofariki Waendelee Kupokea Thawabu
‘Amali za mwana Aadam zinakatika baada ya kufariki kwake isipokuwa matatu kama alivyosema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
Anasema Allaah سبحانه وتعالى:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَا يَعْصُونَ اللَّهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ))
((Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Allaah kwa Anayowaamrisha, na wanatenda wanayoamrishwa)) [At-Tahriym 6]
'Aliy bin Abi Talhah amepokea kutoka Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما kwamba amesema kuhusu Aayah hii: "Mtiini Allaah سبحانه وتعالى na jiepusheni na kumuasi Allaah سبحانه وتعالى na amrisheni familia zenu kumkumbuka Allaah سبحانه وتعالى ili Allaah سبحانه وتعالى Awaokoe na moto wa Jahannam". [At-Twabariy 23: 491]