Zingatio
Zingatio La Wiki,
Dereva anakamata funguo za gari na kushtua engine ya gari, taratibu inaondoka na ipo barabarani tukiiona ikiwa kwenye mwendo. Rubani naye akamata usukani na kuirusha ndege hewani huku sisi ardhini tukiikodolea macho mithili ya udogo wa chembe ya mchanga hali ya kuwa ni yenye kusheheni mizigo au iliyojaa abiria walio wengi tu. Kama kweli twaamini ya kwamba ndani ya gari yupo dereva na ndani ya ndege yupo rubani, kwa nini tusikinaike kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ndiye Bwana wa Ulimwengu?
<?xml encoding="utf-8" ?>
Zingatio: Kila Mtu Ataingia Jannah Isipokuwa Anayekataa
Naaswir Haamid
ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ
“Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema” [Suraatut-Takaathur - 102:8]
Tumekuwa tunakutana ndani ya boksi zetu za barua pepe na barua za ajabu ajabu ambazo imefikia Waislam kutuma picha za wanawake walio uchi sehemu za miili yao zikionekana na maumbile yao ya kushtusha. Muislam akituma mambo kama hayo akiweka kichwa cha habari bila staha wala khofu, ‘mambo hayo’ au maneno kama hayo ya kushabikia uchafu.
Ni jambo la kushangaza kuona ndugu wa Kiislamu wakitumia mambo yenye kushabihiana na itikadi zisizo sahihi, ambayo hayana msingi thabiti wa itikadi sahihi anazotakiwa kuzifuata Muislamu.
Ni mengi ambayo tumeelezwa ndani ya Qur-aan na Sunnah kwa lengo la kupata uongofu. Lakini ni wachache mno wanoelewa hayo. Hata kwa wanaosadiki ukweli huu, kwa namna fulani wanashindwa kuyatekeleza kwa matendo.
Toba ni kuwacha madhambi yote na kujuta kwa kila dhambi Muislamu aliyoifanya, pamoja na kuwa na azma ya kutorudia tena kutenda dhambi hiyo. Wala Muislamu aliyeamini Siku ya Qiyaamah asitosheke na hayo tu, bali aelewe kwamba hana uhakika wa 100% kwamba toba yake imekubaliwa ama laa. Hivyo, ni wajibu wake kuendelea kuwa na matarajio tu na unyenyekevu wa hali ya juu.