Tekeleza Sunnah Ya Kukithirisha Swiyaam Katika Mwezi Wa Sha’baan
Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akikithirisha kufunga (Swiyaam) katika mwezi wa Sha’baan kuliko miezi mengineyo:
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: (كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَصُومُ حَتَّى نَقُولَ لَا يُفْطِرُ، وَيُفْطِرُ حَتَّى نَقُولَ لَا يَصُومُ، وَمَا رَأَيْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم اِسْتَكْمَلَ صِيَامَ شَهْرٍ قَطُّ إِلَّا رَمَضَانَ، وَمَا رَأَيْتُهُ فِي شَهْرٍ أَكْثَرَ مِنْهُ صِيَامًا فِي شَعْبَانَ) مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akifunga hadi tunasema kuwa hatofungua; na anakula (huwa hafungi) hadi tunasema kuwa hatofunga. Sikuwahi kumuona Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) anafunga mwezi mzima bila kufungua isipokuwa mwezi wa Ramadhwaan tu, na sikumuona anafunga sana katika mwezi wowote zaidi ya Sha’baan.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na pia,
عن عَائِشَةَ ـ رضى الله عنها ـ حَدَّثَتْهُ قَالَتْ، لَمْ يَكُنِ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يَصُومُ شَهْرًا أَكْثَرَ مِنْ شَعْبَانَ، فَإِنَّهُ كَانَ يَصُومُ شَعْبَانَ كُلَّهُ، وَكَانَ يَقُولُ (خُذُوا مِنَ الْعَمَلِ مَا تُطِيقُونَ، فَإِنَّ اللَّهَ لاَ يَمَلُّ حَتَّى تَمَلُّوا) وَأَحَبُّ الصَّلاَةِ إِلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم مَا دُووِمَ عَلَيْهِ، وَإِنْ قَلَّتْ " وَكَانَ إِذَا صَلَّى صَلاَةً دَاوَمَ عَلَيْهَا.
‘Aaishah (رضي الله عنها) amehadithia kwamba: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakufunga mwezi wowote zaidi ya kufunga mwezi wa Sha’baan. Alikuwa akisema: ((Fanyeni amali ambazo mnaziweza kwa wepesi, kwani Allaah Hachoki (kulipa thawabu) mpaka nyinyi muwe na ajizi na mchoke (kutenda ‘amali njema)). Na Swalaah bora kabisa aipendayo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni ile inayodumishwa (maishani mwa mtu), japo kama (Swalaah zenyewe) ni chache. Na alikuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) anaposwali Swalaah (za ziyada) alikuwa akizidumisha.” [Al-Bukhaariy]
Na pia,
عَنْ عَائِشَةَ، قَالَتْ لَقَدْ كَانَتْ إِحْدَانَا تُفْطِرُ فِي رَمَضَانَ فَمَا تَقْدِرُ عَلَى أَنْ تَقْضِيَ حَتَّى يَدْخُلَ شَعْبَانُ وَمَا كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَصُومُ فِي شَهْرٍ مَا يَصُومُ فِي شَعْبَانَ كَانَ يَصُومُهُ كُلَّهُ إِلاَّ قَلِيلاً بَلْ كَانَ يَصُومُهُ كُلَّهُ .
‘Aaishah (رضي الله عنه) amesema: “Tulikuwa kati yetu (wanawake) tukifungulia Ramadhwaan, na hutokea kuwa hawezi mtu kulipa deni lake mpaka inapoanza Sha’baan. Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuwa akifunga mwezi wowote zaidi kama alivyokuwa akifunga Sha’baan, alikuwa akifunga wote isipokuwa siku chache. bali alikuwa akifunga (mwezi) wote.” [Sunan An-Nasaaiy]
Sababu Za Swiyaam Mwezi Wa Sha’baan: