<?xml encoding="utf-8" ?>
Fiqh Ya Swawm Ya Ramadhwaan
Kutoka Kitabu 'Al-Wajiyz Fiy Fiqhis-Sunnah Wal-Kitaabil-'Aziyz
Ramadhaan-Swawm
<?xml encoding="utf-8" ?>
Fiqh Ya Swawm Ya Ramadhwaan
Kutoka Kitabu 'Al-Wajiyz Fiy Fiqhis-Sunnah Wal-Kitaabil-'Aziyz
<?xml encoding="utf-8" ?>
Mwezi Wa Ramadhwaan Imeteremshwa Qur-aan
Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan
Nyakati Tatu Muhimu Za Kufanya 'Ibaadah Zisikupite Katika Ramadhwaan
Japokuwa nyakati zote za siku katika mwezi wa Ramadhwaan ni tukufu, ila nyakati hizi tatu ni muhimu mno za kutekeleza ‘ibaadah kutokana na fadhila zake adhimu. Mwenye kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose khaswa katika mwezi huu mtukufu Wa Ramadhwaan ambao ni mwezi wenye malipo maradufu.
1-Wakati wa mwanzo: Baina ya Alfajiri na jua kuchomoza:
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaamrisha kumsabbih katika wakati huu kama Anavyosema:
وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِ﴿٣٩﴾
Na sabbih kwa Himidi za Rabb wako kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa. [Qaaf: 39]
وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا ۖ
Na sabbih kwa Himidi za Rabb wako kabla ya kuchomoza jua, na kabla kukuchwa kwake. [Twaahaa: 130].
Pia, usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh Muslim (564/1) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba walikuwa...
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾
Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa. [Al-Baqarah: 183]
Allaah Anajulisha katika Aliyoyafadhilisha kwa waja Wake kwamba Amewajibisha Swawm kama Alivyowajibisha ummah zilizopita kwa sababu ni shariy’ah (hukmu) na amri zinazomnufaisha bin Aadam katika kila zama.
Nayo ni changamoto ya kumhuisha mtu nafsi yake kwani inapasa kushindana na wengine katika mambo ya khayr ili mkamilishe 'amali zenu na mkimbilie (kuchuma) sifa njema na hakika hayo si katika mambo mazito mliyohusishwa nayo.
Kisha Allaah Anataja hikma Yake kuhusu Shariy’ah ya Swawm, Anasema:
لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
mpate kuwa na taqwa
kwamba Swawm ni sababu kuu ya taqwa (kumcha Allaah) kwa kuwa ni kutekeleza amri za Allaah na kujiepusha na yaliyokatazwa.
Kwa hiyo katika Swawm yanapatikana yafuatayo:
<?xml encoding="utf-8" ?>
Mambo Muhimu Mwenye Swawm Anapaswa Ayajue Kuhusu Swiyaam
Abuu 'Abdillaah
بسم الله الرحمن الرحيم
<?xml encoding="utf-8" ?>
Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah
Kila amali njema atendayo Muislamu inalipwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) mara kumi yake, isipokuwa Swawm ambayo malipo yake ni makhsusi kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama ilivyothibiti katika Hadiyth:
<?xml encoding="utf-8" ?>
Soko La Ramadhwaan Hiloo Linafunguliwa
Na Karibu Kufungwa!
Muhammad Faraj Saalim As-Sa’ay (Rahimahu-Allaah)
Njia 10 Za Kuukaribisha Vizuri Mwezi Mtukufu Wa Ramadhwaan
Inatupasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa) kwa kutupa umri tukiwa katika Uislamu na Iymaan hadi kutufikisha tena kukaribia Mwezi mtukufu wa Ramadhwaan. Na hii ni fursa nyingine Anayotupa Allaah Ta’aala katika maisha yetu kushuhudia mwezi huu na kupata fadhila zake.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾
Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa.
أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ
(Swiyaam ni) Siku za kuhesabika. [Al-Baqarah: 183-184]
Hii ni neema ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa) Ambaye Ametujaalia kuwa na miezi iliyo bora kuliko miezi mingine au siku bora au masaa bora kuliko mengine, ambazo thawabu zake za mema yanayotendeka humo huwa ni zaidi ya nyakati nyingine. Mfano wake, (na Allaah Ana Mifano bora kabisa kulikoni ya yote) ni kama kunapokuwa na mauzo yaliyopunguzwa bei dukani (sale), ambayo kawaida yake huwekwa kwa muda mdogo tu maalum. Na muda huu mtu huweza kununua vitu vingi kwa malipo kidogo tu. Basi Ramadhwaan ni mwezi mmoja tu, lakini malipo yake huwa ni mengi kuliko hata malipo ya miezi yote mingine. Ikiwa mtu atatimiza Swawm yake inavyopaswa na kufanya mema mengi, na akawa katika twaa'ah (utiifu) kamili, taqwa na kuomba maghfirah, basi Muislamu hutoka katika mwezi huu akiwa amechuma thawabu tele na ameghufuriwa madhambi yake.
Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):