Hajj
Hajj
<?xml encoding="utf-8" ?>
<?xml encoding="utf-8" ?>
Makosa Yanayofanywa Baada Ya Kumaliza Hajj na Kurudi Nyumbani
(Kutoka Kitabu Cha Alhidaayah Katika Manaasik Za Hajj Na ‘Umrah)
Mdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) Kwa Wingi Na Omba Maghfirah
Baada Ya Kutenda Mema Katika Siku Kumi Bora Kabisa Za Allaah
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)
وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ ۚ
Na mdhukuruni Allaah katika siku za kuhesabika. [Al-Baqarah:203]
Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kasema: "Siku zinazohisabiwa ni siku za Tashriyq" (11, 12, 13 Dhul-Hijjah) [Al-Qurtwubiy: 3.3] Kwa maana ni siku ya pili, ya tatu na ya nne baada ya siku ya 'Iyd.
Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) baada ya kusherehekea siku kuu yetu ya 'Iydul-Adhwhaa ('Iyd ya kuchinja) ni amri Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Na hivi ndivyo ilivyo desturi ya ‘ibaadah zetu kuwa zinamalizika kwa kuambatana na mema na si kwa maasi.
Mahujaji wanapotekeleza Hajj ipasavyo na wanapomaliza kisimamo cha 'Arafah, huwa wameghufuriwa madhambi yao kama ilivyotajwa katika Hadiyth ifuatayo:
Ratiba Ya ‘'Ibaadah Za Kutekeleza Siku Tukufu Ya ‘Arafah
Ibaadah Za Siku Moja Kwa Malipo Matukufu Mno!
Kabla ya yote, weka niyyah safi kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kutekeleza ‘ibaadah hizi na pia omba du’aa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akujaalie tawfiyq ya kuweza kutekeleza ‘ibaada Siku hii tukufu ya ‘Arafah bila ya kushindwa au kulegea kwa sababu fadhila zake ni tukufu mno.
Hakika hii sio siku ya kutoka nje kuzurura au kutembelea watu, wala sio siku ya kwenda madukani wala sio siku ya kustarehe, bali sio siku ya kujishughulisha na lolote lile isipokuwa kubakia nyumbani au Msikitini kwa wanaume na kubakia katika kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) na kutekeleza 'Ibaadah makhsusi za siku hii tukufu.
1-Lala mapema usiku wake; Yaani tarehe 8 Dhul-Hijjah. Weka niyyah moyoni kufunga (Swawm) Siku ya ‘Arafah ufutiwe madhambi ya miaka miwili kutokana na Hadiyth:
عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه أن النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ : ((صِيَامُ يَوْمِ عَرَفَةَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ وَالسَّنَةَ الَّتِي بَعْدَهُ )) أخرجه مسلم
Abuu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swawm ya 'Arafah nataraji (kwa Allaah) kufuta madhambi ya mwaka uliopita na wa baada yake)) [Muslim]
2-Amka mapema kabla ya alfajiri kwani kuna fadhila tele za kuamka usiku kufanya ‘ibaadah, miongoni mwazo ni zifuatazo:
Allaah (‘Azza wa Jalla) Huteremka hadi mbingu ya dunia kututakabalia du’aa, kutukidhia haja na kutughufuria dhambi kama ilivyotajwa katika Hadiyth ifuatayo:
<?xml encoding="utf-8" ?>
Kuchinja - Fadhila, Hikmah Na Hukmu Zake
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa):
فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾
Fadhila Za Siku Ya 'Arafah Na Yawmun-Nahr (Siku Ya Kuchinja)
‘Arafah ni jabali ambalo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisimama katikati ya bonde lake kuhutubia Maswahaba katika Hajjatul-widaa’i. (hajj ya kuaga), na hapo ndipo wanaposimama Mahujaji kutimiza fardhi ya Hajj. Kusimama hapo ndio nguzo mojawapo kuu ya Hajj. Bila ya kusimama ‘Arafah hijjah ya mtu itakuwa haikutimia kwa dalili ifuatayo:
عن عبد الرحمن بن يعمر قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((الْحَجُّ عَرَفَة، مَنْ جَاءَ قَبْلَ طُلُوعِ الْفَجْرِ مِنْ لَيْلَةِ جَمْعٍ فَقَدْ أَدْرَكَ الْحَجّ)) صحيح الجامع
‘Abdur-Rahmaan bin Ya’mur (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Al-Hajj ni ‘Arafah, atakayekuja kabla kutoka Alfajiri usiku wa kujumuika atakuwa ameipata Hajj)) [Swahiyh Al-Jaami’].
Fadhila Za Siku ya ‘Arafah:
Fadhila Za ‘Umrah Na Hajj
Kutoka Kitabu: Alhidaaya Katika Manaasik Za Hajj Na 'Umrah
Kuna fadhila nyingi zinazopatika kwa kutekeleza ‘ibaadah hizi tukufu. Muislamu anayetaka kuzipata fadhila hizo, lazima afuate amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:
الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَّعْلُومَاتٌ ۚ فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ ۗ وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ وَتَزَوَّدُوا فَإِنَّ خَيْرَ الزَّادِ التَّقْوَىٰ ۚ وَاتَّقُونِ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٧﴾
((Hajj ni miezi maalumu. Na atakayekusudia kuhiji (akahirimia), basi asifanye tendo la ndoa wala ufasiki wala mabishano katika Hajj. Na lolote mlifanyalo katika ya kheri Allaah Analijua. Na chukueni masurufu. Na hakika bora ya masurufu ni taqwa. Na nicheni Mimi enyi wenye akili!)) [Al-Baqarah: 2: 1971]
Kadhaalika, kuna fadhila nyinginezo kadhaa ambazo Muislamu anafaidika nazo zinazohusu Dini na dunia yake: Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
لِّيَشْهَدُوا مَنَافِعَ لَهُمْ وَيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّـهِ فِي أَيَّامٍ مَّعْلُومَاتٍ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّن بَهِيمَةِ الْأَنْعَامِ ۖ فَكُلُوا مِنْهَا وَأَطْعِمُوا الْبَائِسَ الْفَقِيرَ ﴿٢٨﴾
((Ili washuhudie manufaa yao; na walitaje Jina la Allaah katika siku maalumu kwa yale Aliyowaruzuku kati ya wanyama wenye miguu minne wa mifugo. Basi kuleni humo, na lisheni mwenye shida fakiri.)) [Al-Hajj 22: 28]
Aayah hii imetaja baadhi ya manufaa ya ki-Dini na ya kidunia. Ya ki-Dini ni kujichumia thawabu tele katika kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kwenye masiku machache matukufu yaliyojaa fadhila adhimu. Ama manufaa ya kidunia yaliyotajwa humo ni mnyama wa kafara ambaye nyama yake inagaiwa kwa masikini. Manufaa mengineyo ni kama yafuatayo:
<?xml encoding="utf-8" ?>
Mazingatio Na Mafunzo Ya Hajj
Kutoka Kitabu Cha: Alhidaayah Katika Manaasik Za Hajj Na ‘Umrah
Umuhimu Wa Kukimbilia Kutekeleza Nguzo Ya Hajj
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
إِنَّ أَوَّلَ بَيْتٍ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِي بِبَكَّةَ مُبَارَكًا وَهُدًى لِّلْعَالَمِينَ ﴿٩٦﴾
96. Hakika nyumba ya awali iliyowekwa kwa ajili ya watu (kufanya ‘ibaadah) ni ile ambayo iko Bakkah (Makkah), yenye barakah na mwongozo kwa walimwengu.
فِيهِ آيَاتٌ بَيِّنَاتٌ مَّقَامُ إِبْرَاهِيمَ ۖ وَمَن دَخَلَهُ كَانَ آمِنًا ۗ وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴿٩٧﴾
97. Ndani yake kuna Aayaat (ishara, dalili) zilizo wazi; mahali pa kisimamo cha Ibraahiym. Na mwenye kuingia humo anakuwa katika amani. Na kwa ajili ya Allaah ni wajibu kwa watu watekeleze Hajj katika Nyumba hiyo kwa mwenye uwezo. Na atakayekufuru, basi hakika Allaah ni Mkwasi kwa walimwengu. [Aal-‘Imraan 96-97]
Na kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
عن أبي عَبْدِ الرَّحْمنِ عَبْدِ اللهِ بنِ عُمَرَ بنِ الخَطابِ رَضيَ اللهُ عنهُما قال: سَمِعْتُ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم يقولُ: ((بُنَي الإسلامُ على خَمْسٍ: شهادَةِ أَنْ لا إلهَ إلا اللهُ وأَنَّ محمَّداً رسولُ اللهِ، وإقَامِ الصَّلاةِ، وإيتَاءِ الزَّكاةِ، وحَجِّ البَيْتِ، وصَوْمِ رَمَضَانَ )) رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu 'Abdir-Rahmaan 'Abdullaah bin 'Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Uislamu umejengwa kwa nguzo tano: Kukiri na kushuhudia kwamba hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na Muhammad ni Rasuli Wake, kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah na kuhiji Al-Bayt (Makkah) na kufunga swawm Ramadhwaan.” [Al-Bukhaariy na Muslim]
Tunatambua kutokana na kauli hizo kuwa kutekeleza Hajj ni fardhi kwa kila mwenye uwezo. Hivyo asiyeharakisha kutekeleza fardh hii atakuwa amemuasi Rabb wake na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na itakuwa ni dhambi kubwa kwake ikiwa kuacha huko ni kwa makusudi na hali alikuwa ana uwezo wa mali, siha n.k., sababu atakuwa amekanusha amri ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
