Tukumbushane
Imeandaliwa Na 'Abdullaah Mu'aawiyah (Abu Baasim)
Alhidaaya.com
Iymaan-Taqwa
Tukumbushane
Imeandaliwa Na 'Abdullaah Mu'aawiyah (Abu Baasim)
Alhidaaya.com
<?xml encoding="utf-8" ?>

Imekusanywa na: Ummu Iyyaad
<?xml encoding="utf-8" ?>

Imekusanywa na: Ummu Iyyaad
Je, Unampenda Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Ipasavyo Ili Upate Mapenzi ya Allaah?
Hakuna Muislamu asiyekiri kuwa Anamependa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwani hakuna mapenzi yaliyo muhimu kabisa kama mapenzi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ambaye tunamtegemea na kumhitaji kwa mambo yetu yote.
Jambo la kukupeleka kupata mapenzi ya Allaah Amelithibitisha Mwenyewe Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika kauli Yake:
قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٣١﴾
“Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu” [Aal-‘Imraan 3: 31].
Swali kwa kila Muislamu ni: “Je, unamfuata kikweli Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)?” Kwa maana; kufuata aliyoyaamrisha na kuachana na aliyoyakataza?
Jibu la Swali hili ni moja tu hakuna la pili yake. Nalo ni:
Baadhi Ya Amali Na Mambo Yanayosababisha Kupata Mapenzi Ya Allaah (سبحانه وتعالى)
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Atakapompenda mja Wake, basi hakika itatangazwa mbinguni na ardhini na hapo kila kiumbe mwema atakupenda na kila jambo lako litakuwa lenye mafanikio, na pindi Akikuchukia basi kila kiumbe mwema atakuchukia. Hadiyth zifuatazo zimethibitisha:
عن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أَحَبَّ اللهُ تَعَالَى العَبْدَ ، نَادَى جِبْريلَ : إنَّ الله تَعَالَى يُحِبُّ فُلاناً ، فَأَحْبِبْهُ ، فَيُحِبُّهُ جِبريلُ ، فَيُنَادِي في أَهْلِ السَّمَاءِ : إنَّ اللهَ يُحِبُّ فُلاناً ، فَأحِبُّوهُ ، فَيُحِبُّهُ أهْلُ السَّمَاءِ ، ثُمَّ يُوضَعُ لَهُ القَبُولُ في الأرْضِ )) متفق عليه
.
وفي رواية لمسلم : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ الله تعالى إذا أحب عبداً دعا جبريلَ ، فقال : إنّي أُحِبُّ فلاناً فأحببهُ ، فيحبُّهُ جبريلُ ، ثمَّ ينادي في السماءِ ، فيقول : إنَّ اللهَ يحبُّ فلاناً فأحبوهُ ، فيحبُّهُ أهلُ السماءِ ، ثمَّ يوضعُ لهُ القبولُ في الأرضِ ، وَإِذَا أبْغَضَ عَبْداً دَعَا جِبْريلَ ، فَيَقُولُ : إنّي أُبْغِضُ فُلاناً فَأبْغِضْهُ . فَيُبغِضُهُ جِبريلُ ثُمَّ يُنَادِي في أَهْلِ السَّماءِ : إنَّ الله يُبْغِضُ فُلاناً فَأبْغِضُوهُ ، ثُمَّ تُوضَعُ لَهُ البَغْضَاءُ في الأَرْضِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anapompenda mja anamuita Jibriyl na kumwambia: “Hakika Mimi nampenda fulani, hivyo nawe mpende.” Hivyo Jibriyl anampenda mtu huyo na baada ya hapo anatangaza kwa watu wa mbinguni kwamba: ‘Hakika Allaah anampenda fulani, kwa hivyo nanyi nyote mpendeni.’ Hapo watu wa mbinguni wanampenda mtu huyo. Kisha anawekewa kabuli (kukubaliwa) na watu wa ardhini. [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na katika riwaayah ya Muslim: Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anapompenda mja, anamuita Jibriyl, na kumwambia: “Hakika Mimi nampenda fulani, nawe mpende.” Hivyo Jibriyl anampenda mtu huyo na baada ya hapo anatangaza mbinguni kwa kusema: ‘Hakika Allaah Anampenda fulani, kwa hivyo nanyi nyote mpendeni.’ Hapo watu wa mbinguni nao pia wanampenda mtu huyo. Kisha anawekewa kabuli (kukubaliwa) na watu wa ardhini. Na Allaah Anapomchukia mtu yeyote anamuita Jibriyl na kumwambia: “Hakika Mimi namchukia fulani, nawe mchukie.” Hivyo Jibriyl (‘Alayhis-salaam) anamchukia mtu huyo na baada ya hapo anatangaza kwa watu wa mbinguni kwamba: “Hakika Allaah Anamchukia fulani, kwa hivyo nanyi nyote mchukieni.” Hapo watu wa mbinguni nao pia wanamchukia mtu huyo. Kisha anawekewa chuki na watu wa ardhini.”
Na pindi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akikupenda, basi utakuwa katika ulinzi Wake na kila adui yako atakuwa ni adui wa Allaah ('Azza wa Jalla) na Atakutaqabalia haja zako:
عن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ الله تَعَالَى قَالَ : مَنْ عَادَى ليَ وَلِيّاً ، فَقَدْ آذَنْتُهُ بِالحَرْبِ ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدِي بِشَيءٍ أَحَبَّ إِلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيهِ ، وَمَا يَزالُ عَبْدِي يَتَقَرَّبُ إِلَيَّ بِالنَّوَافِلِ حَتَّى أُحِبَّهُ ، فَإِذَا أحْبَبْتُهُ ، كُنْتُ سَمْعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بِهِ ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بِهِ ، ويَدَهُ الَّتي يَبْطِشُ بِهَا ، وَرجْلَهُ الَّتِي يَمْشِي بِهَا وَإنْ سَألَنِي أعْطَيْتُهُ ، وَلَئِن اسْتَعَاذَنِي لأعِيذَنَّهُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa Amesema: "Mwenye kumfanyia uadui rafiki yangu basi Nimemtangazia vita. Hajikurubishi Kwangu mja Wangu kwa kitu ninachokipenda zaidi kuliko nilichomfaradhishia, Na mja haachi kujikurubishi kwangu kwa Sunnah mpaka Nimpende. Ninapompenda, Ninakuwa sikio lake analosikilizia, na jicho lake analoonea, na mkono wake anaoshikia, na mguu wake anayotembelea, Akiniomba Nitampa, na akijilinda kwangu Nitamlinda." [Al-Bukhaariy]
Basi jitahidi upate mapenzi ya Allaah ('Azza wa Jalla) kwa kutekeleza yafuatayo:
Fadhila Za Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Na Vipi Kumswalia
Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:
إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ ۚ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾
Hakika Allaah na Malaika Wake wanamswalia Nabiy. Enyi walioamini mswalieni na msalimieni kwa mamkizi ya amani na kwa tasliymaa. [Al-Ahzaab (33: 56)]
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ ۚ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾
Hakika Allaah na Malaika Wake wanamswalia Nabiy. Enyi walioamini mswalieni na msalimieni kwa maamkizi ya amani na kwa tasliymaa. [Al-Ahzaab 33: 56]
Maana ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Ni kumsifia kwa Malaika, kumteremshia rahmah na baraka, fadhila n.k.
Maana ya Malaika Wake kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni kumuombea kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) du’aa Amghufurie na Amteremshie baraka.
Maana ya Waumini kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni kumuombea kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) du’aa na amani. Juu ya hivyo Waumini kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inawarudia wenyewe thawabu tele kutokana na fadhila zilizotajwa katika Hadiyth kadhaa za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), miongoni mwazo ni:
Fadhila Za Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
1-Kupata thawabu mara kumi kwa kumswalia mara moja:
عنْ عبد اللَّه بن عمرو بن العاص رضي اللَّه عنْهُمَا أنَّهُ سمِع رسُول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقُولُ: ((مَنْ صَلَّى عَلَيَّ صَلاَةً، صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ بِهَا عشْراً)) رواهُ مسلم
Imetoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru bin Al'-Aasw (رضي الله عنهما) kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Atakayeniswalia mara moja, Allaah Atamswalia mara kumi)) [Muslim]
2-Kupata ukaribu wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Peponi:
Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharram, Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake
AlhamduliLLaah, Tunamshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaaa) Kutufikisha tena katika mwaka mwengine mpya wa Kiislamu. Mwezi wa Al-Muharram una fadhila makhsusi kulingana na miezi mitukufu mingineyo. Moja wa fadhila hizo ni funga ya tarehe 9 na 10 Al-Muharram zinazojulikana kama Taasu'aa na 'Aashuraa. Hivyo ndugu Waislamu tusiache kufunga siku hizi mbili kwani thawabu zake ni kufutiwa madhambo ya mwaka mzima!
قال النبي صلى الله عليه وسلم: ((صِيامُ يَوْمِ عَاشُورَاءَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ)) رواه مسلم
Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swawm ya siku ya 'Aashuraa, nataraji kutoka kwa Allaah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia)) [Muslim]
Bonyeza viungo vifuatavyo:
Nasiha Na Ukumbusho Wa Swawm Siku Ya Taasu'aa (9) Na 'Aashuraa (10)
Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾
Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo, (iko miezi) minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu (kwa kufanya maasi), na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]
Na Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema katika Hadiyth:
عن أبي بَكْرَةَ رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أنه قَالَ: إن الزَّمَانَ قَدْ اسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْمَ خَلَقَ اللَّهُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ السَّنَةُ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ثَلاثٌ مُتَوَالِيَاتٌ ذُو الْقَعْدَةِ وَذُو الْحِجَّةِ وَالْمُحَرَّمُ وَرَجَبُ مُضَرَ الَّذِي بَيْنَ جُمَادَى وَشَعْبَانَ
Imepokelewa kutoka kwa Abu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mgawano wa zama umerudi katika hali yake ya asili siku Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili; minne miongoni ya hiyo ni mitukufu, mitatu inafuatana pamoja; Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Al-Muharram, mwengine ni Rajab wa (kabila la) Mudhwarr ambao uko baina ya Jumaadaa na Sha'baan)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Faida Kuhusu Mwezi Wa Al-Muharram
1-Swawm (funga) yake ni swawm bora kabisa baada ya Ramadhwaan:
<?xml encoding="utf-8" ?>
Ukimdhukuru Allaah Naye Atakukumbuka
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):