أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com
048-Al-Fat-h: Aayah 1 - 5
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾
Hakika Tumekupa ushindi (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), ushindi bayana.
لِّيَغْفِرَ لَكَ اللَّـهُ مَا تَقَدَّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ وَيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿٢﴾
Ili Allaah Akughufurie yale yaliyotangulia katika madhambi yako na yale yanayofuatia; na Akutimizie neema Yake juu yako na Akuongoze njia iliyonyooka.
وَيَنصُرَكَ اللَّـهُ نَصْرًا عَزِيزًا﴿٣﴾
Na Akunusuru Allaah nusura yenye nguvu kabisa.
هُوَ الَّذِي أَنزَلَ السَّكِينَةَ فِي قُلُوبِ الْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُوا إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ ۗ وَلِلَّـهِ جُنُودُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٤﴾
Yeye Ndiye Aliyeteremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili Awazidishie iymaan pamoja na iymaan zao. Na ni ya Allaah Pekee majeshi ya mbinguni na ardhini, na Allaah ni daima Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.
لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾
Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu.
[[Al-Fat-h: 1 – 5]
Sababun-Nuzuwl:
عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه قَالَ لَمَّا نَزَلَتْ: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُبِينًا * لِيَغْفِرَ لَكَ اللَّهُ)) إِلَى قَوْلِهِ: ((فَوْزًا عَظِيمًا)) مَرْجِعَهُ مِنَ الْحُدَيْبِيَةِ وَهُمْ يُخَالِطُهُمُ الْحُزْنُ وَالْكَآبَةُ وَقَدْ نَحَرَ الْهَدْىَ بِالْحُدَيْبِيَةِ فَقَالَ " لَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَىَّ آيَةٌ هِيَ أَحَبُّ إِلَىَّ مِنَ الدُّنْيَا جَمِيعًا " .
Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema: Ilipoteremka:
إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾
Mpaka kauli Yake:
فَوْزًا عَظِيمًا
Alipokuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na Maswahaba wanarudi kutoka Hudaybiyah wakiwa katika hali ya kuzidiwa na ghadhabu, huzuni na dhiki (kwa kuzuiliwa na Makafiri Quryash kuingia Makkah) Wakawa wamechinja Hady (mnyana wa Hajj) wao. (Hapo zikateremshwa Aayah hizo) na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika nimeteremshiwa Aayah ambazo ni vipenzi zaidi kuliko dunia nzima.” [Muslim Kitaab Al-Jihaad Was Sayr]
Pia,
عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا)) قالَ الْحُدَيْبِيَةُ. قَالَ أَصْحَابُهُ هَنِيئًا مَرِيئًا فَمَا لَنَا? فَأَنْزَلَ اللَّهُ : ((لِيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ)) قَالَ شُعْبَةُ فَقَدِمْتُ الْكُوفَةَ فَحَدَّثْتُ بِهَذَا كُلِّهِ عَنْ قَتَادَةَ ثُمَّ رَجَعْتُ فَذَكَرْتُ لَهُ فَقَالَ أَمَّا: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ)) فَعَنْ أَنَسٍ، وَأَمَّا هَنِيئًا مَرِيئًا فَعَنْ عِكْرِمَةَ.
Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema kuhusu:
إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا
Inahusiana na (Bay’ah) ya Hudaybiyah. Maswahaba wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wakasema kumwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Hongera na furaha kwako, lakini je sisi tunapata nini?” Hapo Allaah Akateremsha:
لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾
Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu. [Al-Bukhaariy]
Pia,