'Amaar Bin Yaasir (Radhwiya Allaahu 'anhu) Ukoo wote wa Yaasir baba yake 'Ammaar (Radhwiya Allaahu 'anhum) ulipata bahati ya kubashiriwa na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuingiia Peponi. Yaasir (Radhwiya Allaahu 'anhu) alisafiri kutoka kwao Yemen kwa ajili ya kumtafuta ndugu yake aliyepotea miaka mingi. Alipofika Makka akaamua kuishi hapo chini ya Himaya ya Abu Hudhayfah aliyemwozesha mmoja katika vijakazi wake aitwae Summayyah binti Khayat (Radhwiya Allaahu 'anhaa), na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) akawaruzuku mtoto mwema waliyempa jina la 'Ammaar.