Tanabahi Kuhusu Bid'ah Za Niswfu Sha’baan; Swawm, Adkhaar Na Kuomba Du’aa
Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi waa alihi wa sallam) ametahadharisha kuhusu bid’ah aliposema:
((أُوصِيكُمْ بِتَقْوى اللَّه، وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وإِنْ تَأَمَّر عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حبشيٌ، وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيرى اخْتِلافاً كثِيرا. فَعَلَيْكُمْ بسُنَّتي وَسُنَّةِ الْخُلُفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ، عضُّوا عَلَيْهَا بالنَّواجِذِ، وإِيَّاكُمْ ومُحْدثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَ بِدْعَةٍ ضلالَةٌ)) رواه أبو داود، والترمذِي وقال حديث حسن صحيح
((Nakuusieni kumcha Allaah, usikivu na twaa hata ikiwa kiongozi wenu (Au atakayekuamrishen) ni Mtumwa wa Habash. Mtakaoishi miongoni mwenu mtaona ikhtilafu nyingi. Kwa hiyo shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa waliongoka baada yangu. Ziumeni kwa magego (zikamateni kwa nguvu wala msiziache). Na tahadharini na mambo ya uzushi kwani kila bid'ah ni upotofu)) [Abu Daawuwd, At-Trimidhiy kasema Hadiyth Hasan Swahiyh]
Na katika Riwaayah nyingine alikuwa kila alipokhutubia akitanguliza kusema:
أَمَّا بَعْدُ ، فَإِنَّ خَيْرَ اَلْحَدِيثِ كِتَابُ اَللَّهِ ، وَخَيْرَ اَلْهَدْيِ هَدْي ُ مُحَمَّدٍ ، وَشَرَّ اَلْأُمُورِ مُحْدَثَاتُهَا، وَكُلَّ بِدْعَةٍ ضَلَالَة ، رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Ammaa Ba’du, Hakika Maneno bora kabisa ni Kitabu cha Allaah (Qur-aan) na mwongozo bora kabisa ni mwongozo wa Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم), na uovu zaidi wa mambo ni yale yenye kuzushwa (bila dalili ya kisharia), na kila bid'ah ni upotofu. [Muslim]
Swali:
“Je, bid’ah, hata bid’ah hiyo iwe ndogo vipi ni miongoni mwa madhambi makubwa? Au kuna ufafanuzi bayana wa hili?”
Jibu: