Vile vile inaruhusiwa kufanya Tayammum mara nyingine badala ya wudhuu kabla ya kulala. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Bibi ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema:
كانَ رسولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلّم إذا أجنبَ فأرادَ أنْ ينامَ توضأَ
"Mtume alipokuwa katika hali ya janaba na kila alipotaka kwenda kulala alikuwa akichukua wudhuu au akitayammum".[1]