Swahiyh Fiqh As-Sunnah
كِتَابُ الزَّوَاجِ
Kitabu Cha Ndoa
الحُقُوْقُ بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ
Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume
11: Haki Zinazompasa Mume Kumtendea Mkewe: 8-Ayafumbie Macho Baadhi Ya Makosa Ya Mkewe Madhali Si Yenye Kukiuka Maagizo Ya Allaah:
Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuongoza katika hili akituambia:
"لَا يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إِنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقًا رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ"
“Muumini wa kiume (mume) asimbughudhikie Muumini mwanamke (mkewe). Kama atachukizwa na baadhi ya tabia zake, basi zingine zitamfurahisha”. [Swahiyh Muslim (1469)]