Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الحلف بمخلوق
كالنبي والكعبة والملائكة والسماء والآباء والحياة والروح
والرأس وحياة السلطان ونعمة السلطان وتربة فلان والأمانة ، وهي
من أشدها نهياً
061-Mlango Wa Kukatazwa Kuapa kwa Viumbe Kama Nabiy, Ka'abah, Malaaikah, Mbingu, Baba, Uhai, Roho, Kichwa, Neema ya Sultani, Mchanga wa Fuani (Kaburi) na Amana, Nayo Imekatazwa kwa Ukali Zaidi
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ الله تَعَالَى يَنْهَاكُمْ أنْ تَحْلِفُوا بِآبائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفاً ، فَلْيَحْلِفْ بِاللهِ ، أَوْ لِيَصْمُتْ )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية في الصحيح : (( فَمَنْ كَانَ حَالِفاً فَلاَ يَحْلِفْ إِلاَّ بِاللهِ ، أَوْ لِيَسْكُتْ )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Anawakatazeni kuapia kwa baba zenu, mwenye kuapa basi amuapie Allaah au anyamaze." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن عبد الرحمان بن سَمُرَةَ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَحْلِفُوا بِالطَّوَاغِي ، وَلاَ بِآبَائِكُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abdir-Rahmaan bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usiape kwa Twawaaghiy wala kwa baba zenu." [Muslim]. Twawaaghiyt ni wingi wa Twaaghiyah nayo ina maana ya masanamu. Na miongoni mwayo ni Hadiyth: "Hili ni Twaaghiyah la Daws", yaani ni sanamu lao wanalo liabudu. Na imepokewa katika riwaayah isipokuwa ya Muslim: "Bit Twawaaghiyt", nayo ni mwingi wa Twaaghuwt yenye maana ya shetani na sanamu.
Hadiyth – 3
وعن بُريدَةَ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ حَلَفَ بِالأمَانَةِ فَلَيْسَ مِنَّا )) حديث صحيح ، رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa kama amana si katika sisi." [Hadiyth Swahiyh iliyopokewa na Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 4
وعن بُريدَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ حَلَفَ فَقَالَ : إنِّي بَرِيءٌ مِنَ الإسْلاَمِ ، فَإنْ كَانَ كَاذِباً ، فَهُوَ كمَا قَالَ ، وإنْ كَانَ صَادِقاً ، فَلَنْ يَرْجِعَ إِلَى الإسْلاَمِ سَالِماً )) . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa, akasema: 'Mimi niko mbali na Uislamu, ikiwa ni muongo, basi atakuwa kama alivyosema na akiwa ni mkweli hatarudi katika Uislamu akiwa salama." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 5
وعن ابن عمر رضي الله عنهما: أنَّهُ سَمِعَ رَجُلاً يقُولُ: لاَ وَالكَعْبَةِ، فَقَالَ ابنُ عُمَرَ : لاَ تَحْلِفْ بَغَيْرِ اللهِ ، فَإنِّي سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ حَلَفَ بِغَيرِ اللهِ ، فقد كَفَرَ أَوْ أشْرَكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alisikia mtu akisema: "Naapa kwa Ka'abah." Ibn 'Umar akamwambia: "Usiape kwa asiyekuwa Allaah, kwani nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah, hakika amekufuru au amefanya shirki'." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]